8 Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja
punje thelathini, moja sitini na nyingine mia." (Luka 4:8)
Tunahitaji kuzaa matunda yanayokaa. Katika hali
ya kawaida bila udongo mzuri mazao hayatastawi kabisa. Pasipo udongo mzuri
kukua ni ndoto za abunuasi. Pasipo udongo mzuri tusitegemee nguvu za Mungu.
Pasipo udongo mzuri tusitegemee kujitoa kikamilifu kwa Yesu. Pasipo udongo
mzuri hakuna kujaa na kufurika. Pasipo udongo mzuri tusitegemee uamsho kwa mtu
au kwa kundi. Udongo upo wa aina nyingi. Hata wakulima wanapotaka kupanda mazao
yao hawaendi popote tu wakapanda mbegu. Mkulima mzuri atachagua mahali
panapofaa kwa mbegu zake kuota na kukua.
Je mimi na wewe tupo katika udongo gani? Je
ni mfinyanzi? Je, ni mchanga, Je, ni udongo mzuri?
Maadamu mbegu ni mfano wa mtu, hakuna
bahati mbaya katika kupandwa kwenye udongo usiofaa. Mtu mwenyewe anajipeleka
kwenye udongo mzuri au ule usiofaa. Uchaguzi wa wapi ukapandwe kama mkristo ni
wako wewe mwenyewe.
Ukitaka kukua na kuongezeka au kuzaa unajikita kwenye udongo mzuri. Ukitaka kuwa mkristo wa kawaida bila kuwa na matunda unajikita kwenye mwamba, kwenye miiba au popote pasipokuwezesha kukua na kuongezeka. Hii ni mada endelevu.
Ukitaka kukua na kuongezeka au kuzaa unajikita kwenye udongo mzuri. Ukitaka kuwa mkristo wa kawaida bila kuwa na matunda unajikita kwenye mwamba, kwenye miiba au popote pasipokuwezesha kukua na kuongezeka. Hii ni mada endelevu.
Barikiwa