Wednesday, April 17, 2013

UKRISTO NA DHIKI

mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
 [1 Wathesalonike 3:3]



Katika maeneo magumu sana kwa mkristo anayesafiri ni kukubaliana asilimia mia moja na ukweli halisi wa kimungu kuhusu taabu, shida na dhiki.

Biblia inashangaza pia hata katika waraka wa Yakobo pale unapohimiza watu kuhesabu kuwa ni furaha tupu tunapopita katika majaribu mbalimbali.

Dhiki haipendezi. Dhiki ni ngumu kukubaliana nayo. Baadhi ya mambo nyeti kama kifo yamefichwa kwetu na Mungu. Mungu anajua kwamba kwa akili zetu za kibinadamu hatupendi shida au mateso. Mungu angeweza kuruhusu kwa mamlaka tuliyopewa kwamba, ukiona kuna jaribu wiki kesho basi unaumba kifo wiki hii na unaondoka duniani ili wiki kesho usipate jaribu fulani.

Hata na wale wenye pesa nyingi hawana uwezo wa kukwepa matatizo na dhiki zote. Katika dhiki tunatakiwa kujinyenyekeza kwa Mungu wetu.

Mungu anataka tupitie kwenye dhiki. Tuahitaji kumuomba yeye atuwezeshe kuhesabu kuwa ni furaha tupu kuingia katika majaribu mbalimbali.

No comments:

Post a Comment