Sunday, December 16, 2012

FIMBO YA NGUVU ZAKO


Bwana atainyosha toka sayuni
Fimbo ya nguvu zako
Uwe na enzi kati ya adui zako. (zaburi 110:2)

 

Tunapoendelea kuishi katika maisha ya wokovu au utauwa, tunakutana na vikwazo, milima, visiki, mawe, magonjwa, njaa, kuishiwa, madeni, kuchukiwa, kuonewa, upinzani, kukosa uhuru na mengine mengi. Tunakutana na hayo kwa sababu hayo ni sahemu ya dunia tunayoishi. Hatupandishwi daraja bila kushinda katika hayo. Mwimba zaburi anaposema adui,  analenga vitu vyote nilivyotaja hapo juu. Mengine yameendelea kuwa changamoto kwetu hata wakati ambao tumeyakemea au kuomba yaondoke kabisa.

Pamoja na changamoto za namna moja au nyingine, neno la Mungu linatukumbusha kwamba tunayo fimbo. Hii ni alama ya mamlaka. Fimbo yako ni mamlaka yako. Ahadi imetolewa. Kama ukishaielewa ni ahadi ya jinsi gani na uidai vipi kwa Bwana basi utachangamka. Wewe dai ahadi ya fimbo yenye nguvu.

Fimbo hii itanyoshwa kutoka sayuni, na siyo kutoka Mabwepande au Makambako. Fimbo hii haitanyoshwa kama kubofya rimoti ya TV. Fimbo hii inatafutwa. Fimbo hii inahangaikiwa. Tunajua sana kwamba hata Yesu mwenyewe alisema kwamba ufalme wa Mungu utatekwa na wenye nguvu. Fimbo inanyoshwa kutoka Sayuni. Sayuni ni kwenye maombi. Sayuni ni kwenye ibada. Sayuni ni kwenye sifa. Sayuni ni kwenye maombi ya kujitoa. Sayuni ni kwenye kusoma neno.Sayuni ni katika kutafakari neno na kupata mafunuo.

Vitu nilivyovitaja hapo juu vinashindika tu mbele za Mungu kupitia Mfalme Yesu. Ni hiyo fimbo yenye nguvu inayoleta jibu kwako.

Tafakari

No comments:

Post a Comment