Thursday, December 13, 2012

UTAKATIFU WA KILA SIKU


 

kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu. (Luka1:75)




Mara nyingi sana huwezi kukuta mtu aliyeokoka anfurahia dhambi. Hata hivyo ukweli unabaki palepele kwamba watu wengi tuna utakatifu wa mdomo na si ule wa matendo.

Kusema ukweli limekuwa jaribu kubwa nyakati za leo. Watu ni wakali na hawapendi kuguswa kwenye maeneo ya udhaifu wao.

Utakatifu katika andiko hilo hapo juu ni ule wa siku zote. Utakatifu wa masaa ni kinyume cha biblia. Utakatifu wa wiki siyo neno la Mungu. Utakatifu wa kuimba pambio tu, sicho tulichoitiwa.




Hapatakiwi kuwa na tofauti ya mahali katika suala la utakatifu. Kazini na nyumbani mtu uwe yule yule unayemcha Mungu.

OMBI:

Ee Mungu naomba unijalie kuwa na toba ya kweli kuhusu njia zangu. Naomba unielekeze katika kukuhofu wewe, na kuwa mtakatifu siku zote

No comments:

Post a Comment