Tuesday, December 18, 2012

KUOMBA KWA MUDA MREFU

Ombeni bila kukoma (1 Thes 5:17)

Mtu anapoanza kuokoka tunaweza kumfundisha kuomba au jambo fulani la kiroho kwa kutumia vikanuni na vijisheria fulani. hii ni kwa sababu yeye bado ni mchanga na anahitaji maziwa. Bado anahitaji kuelekezwa taratibu. 

Lakini ukiisha kuwa mzoefu wa maneno ya imani, au umeshakua kiroho haitakiwi ufundishwe kama wanaoanza safarileo. Mbinu ambayo mimi ninaishauri ni kutumia sifa, neno na kuabudu. Ukiwa kwako unaweza ukakesha bila taabu. Andaa tenzi, biblia kalamu daftari. Usiweke sana kanuni kuhusu nini kianze na nini kifuate.

Unafungua kwa maombi mkesha wako. Unaanza kuimba pambio mbalimbali za kusifu. Unafuatisha kuimba nyimbo za kuabudu. Ukiona roho yako imeloana uwepo anza kuomba kwa kufuata jinsi Roho Mtakatifu atakavyokuongoza. Kama ni kunena kwa lugha fuatisha tu. Ukiona umefanya chochote sana mpaka unakuwa kama umechoka acha na uanze kingine. Mfano acha kuomba, ingia kusifu. Hivyohivyo na itafika mahali ambapo hakuna anayeweza kukuzuia. Hapo unaweza kuomba hadi asubuhi. 

Wewe una maoni gani?

BARIKIWA


No comments:

Post a Comment