Thursday, December 13, 2012

UMWONE MUNGU BILA UTAKATIFU?


14 Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo( Waebrania 12:14)

Sisemi kwamba hujui kutubu ee ndugu katika bwana. Sisemi kuimba ni tatizo rafiki. Ila ninachosema ni kwamba, utakatifu wa kumuona Mungu unazingatia amani ya mtu na watu wote. Siku hizi ni vigumu kuhubiri injili ya utakatifu wote makanisani. Watu wako tayari kukuundia vikao vya kufukuzwa kanisani ikiwa tu utahubiri utakatifu kwa viwango vya juu. Watu waliookoka siku hizi tumepoteza sifa na maana ya kuokoka. lokole ndo wanaolalamika sana, hawamtegemei Mungu kama zamani. Hawavai vizuri na kwa heshima tena. Nywele zao huzitengeneza kama watu wa mataifa wanavyotengeneza. Yaani ni kukosa kiasi, ni kulata fujo tu humo makanisani.

Wewe unatengeneza nywele, una amani na Mungu wako sawa sikatai. Lakini hizo nywele ni kwazo kwa wanaokutazama au majirani zako.Pia ni kwazo kwa afya ya ngozi yako. Je amani yako na watu ikoje? unavaa pedo pusher, umejaa Roho Mtakatifu, sina tatizo. Hiyo amani ya pedo pusher kwa watu wote inapatikanaje?

Usifanye kitu kinacho poteza amani na watu wote. Kumbuka siyo mtu mmoja tu, ni watu wote. Suala siyo utakatifu tu, ila ni utakatifu ambatano. (Waebrania 12:14)

barikiwa

No comments:

Post a Comment